Alhamisi, 13 Novemba 2014

michakato ya kimofolojia inavyotumika kuunda maneno katika lugha ya kiswahili.



Mofolojia ni taaluma inayoshughulikia vipashio vya lugha na mpangilio wake katika uundaji wa maneno. Vipashio hivyo vya lugha huitwa mofimu (Rubanza, 1996).
Mofolojia ni tawi la taaluma ya isimu ambalo huchunguza maumbo ya maneno na hususani: maumbo ya mofimu. (Mathews, 1974)
Hartman (1972) anasema kuwa mofolojia ni tawi la sarufi ambalo hushughuliia na uchunguzi na uchambuzi wa maumbo, fani na aina zao maneno yalivyo sasa pamoja na histori zao.
Mofolojia huchunguza mofimu na alomofu zake fulani na jinsi ambavyo hukaa pamoja kuunda maneno mbalimbali katika lugha zinamotumika (Richard na wenzake 1985).
Kwa ujumla, mofolojia ni tawi la isimu ambalo huchunguza maneno ya lugha fulani na aina zake za maneno hasa upande wa upangaji wa mofimu mbalimbali zitumikazo kwa ajili ya kuunda maneno. Pia wana taalamu mbalimbali wamefasili maana ya maneno kwa mitazamo mabalimbali kama ifuatavyo.
Tuki, (1970) Neno ni mkusanyiko wa sauti ambazo huweza kutamukika na kuandikwa kwa pamoja na kuleta maana.
Massamba na wenzake (2003) wanafasi neno kwa kutafasili maelezo ya Lynos (1968:194- 208) kuwa neno linawez kufafanuliwa katika misingi ya kiumbo sauti yaani kwa kuchunguza sauti zinazounda umbo zima, kiontografia kwa kuchunguza herufi zinazotumika katika kuliandaka umbo lake, kisarufi kwa kuchunguza kile kinachowakilishwa na umbo husika katika lugha.
Katika lugha ya Kiswahili, maumbo ya kimatamshi na ya kimaandishi huweza kuwakilisha umbo moja au maumbo kadhaa ya kisarufi. Mfano,  katika lugha ya Kiswahili kuna umbo la Kimaandishi kaa. Kisarufi umbo hili linawakilisha maumbo matatu yenye maana tofauti kama ifuatavyo.
Kaa- tendo la kuketi kitako
Kaa- aina ya samaki
Kaa- kipande cha ukuni chenye moto au kilichochomwa.
Kwa ujumla, neno ni sehemu ya lugha yenye kituo kidogo mbele na nyuma yake, au kwa maandishi ni jumla ya herufi zenye maana zilizotengwa kwa nafsi nyuma na mbele.
Maneno katika lugha ya Kiswahili huweza kuundwa kupitia michakato mbalimbali kama vile kimofolojia, na kifonolojia, kwa kutumia mchakato wa kimofolojia, neno huweza kuundwa kupita kanuni mbalimbali kama vile, udondoshaji, uyeyushaji, Muungano wa sauti, nazali kuathiri konsonanti, konsonanti kuathiri nazali, Ukaakaishaji, usilimishaji au usilimisho na mchato wa msinyao.
Katika mchakato wa udondoshaji, kiambishi awali m- ambacho huonekana katika umbo la nje la maneno kama mu- tu, mu- gonjwa, mu – kanda. Katika kanuni au mchakato huu wa undoshaji. Irabu “u” hudondoshwa pale inapofuatiwa na konsonanti halisi katika mpaka wa mofimu. Mfano.
Mu+ tu= mtu
Mu+ gonjwa= mgonjwa
Mu+ kanda= mkanda
Mu + guu = mguu
Mu + china= mchina
Mu+ kulima = mkulima.
Pia irabu ‘u’ inapokalibiana na irabu inayofanana nayo hubaki kama ilivyo.Mfano
Muumba-  muumba
Muumini- muumuni
Muuguzi- muuguzi
Mungwana- muungwana
Muunguja- muunguja.
Mchakato wa uyeyushaji, kanuni hii hutokea pale irabu inapoandamana na nazali “m” na pale inapokuwa yenyewe. Irabu ‘u’ inapofuatiwa na mofimu inayoanza na irabu inayofanana nayo hubakia jinsi ilivyo lakini inapofuatiwa na irabu isiyofanana nayo wakati mwingine huweza kubakia kama ilivyo au huweza kugeuka na kuwa ‘w’ pia irabu ‘I’ huathiriwa na kanuni hii mfano
Mi+ ake- myaka
Vi+ ake- vyake
Vi+ ao- vyao
Vi+ akula          vyakula
Pia katika kanuni hii neon likitamkwa kwa haraka uyeyushaji huweza kutokea. Mfano;
Mu+e+nde+shaji          mwendeshaji
Mu+i+mba+ji              mwimbaji
Mu+ema                      mwema
Mu+eupe                     mweupe
Katika kanuni hii iwapo kuna namna mbili za utamkaji inaashiria kuwa katika mazingira hayo kanuni ya uyeyushaji ni ya hiyari.
Machakato wa muungano wa sauti, kanuni hii hutokea pale ambapo irabu ya mofimu moja inapokabiliana na irabu ya mofimu nyingine irabu hizo mbili huungana na kuzoa irabuy moja tu mfano
Wa+ ingi- wengi
Me +ingi- mengi
Hapa ina maana kuwa irabu ‘a’ na irabu za mbele yaani ‘i’ na ‘e’ zinapokutana katika mpaka wa mofimu huungana na kuzaa irabu moja tu ‘e; lakini kuna vigaili amabapo hutokea inapokuwa mofimu inayoiandama ina minyambuliko. mfano
Wa+ igi+za+ ji - waigizaji
Wa+ oko+ a+ ji-  waokoaji
Mchakato wa nazali kuathiri konsonanti andamizi, katika kanuni hii baadhi ya sauti ambazo huathiriwa na nazari inapokuwa sauti hizo zinazoindamia nazari hizo. mfano.
                        n+ limi- {ndimi}
n+ refu- {ndefu}
Katika mifano hii inaonekana kwamba sauti/ l/na/r/ zinapotanguliwa na nazari “n” hugeuka na kuwa sauti/d/
Mchakato wa konsonanti kuathiri nazali,katika lugha za kibantu umbo la nazali huathiriwa na konsonanti inayoind amia. kwa mfano
Nguzo- [inguzo]
Ngao-[ ingao ]
Katika mifano hii konsonanti inayofuatia nazali ni “g”. konsonsanti hii hutamkiwa nyuma  kwenye kaakaa laini, kwa maelezo haya….. haitokei hivihivi bali ni kutokana na kanuni hii maalumu ya lugha nyingi za kibantu ambazo ni kanuni ya konsonanti kuathiri nazali. 
Mchakato wa ukaakaishaji  wa fonimu,  hutopkea wakati ambapo fonimu zisizo za kaakaa gumu zionapobadilika na kuwa fonimu za kaakaa gumu. Katika lugha ya kiswahili fonimu za kaakaa gumu ni mbili yaani vizuiwa kwamizwa ambavyo ni ?t? na ?ts? kwa hiyo katika lugha ya kiswahili ukaaishaji wa fonimu hutokea wakati ambapo fonimu zisizo vizuiwa kwamizwa hubadilika na kuwa vizuiwa kwamizwa. Ukaakaishaji katika lugha ya Kiswahili hutokea zaidi katika vivumishi, nomino na vitenzi .
ukaakaishaji katika  vivumishi hutokea  katika mipaka ya mofu  za vivumishi, vivumishi vinavyohusika ni vile ambavyo mizizi huanzia na irabu. Kiambishi awali pekee ambacho husababisha ukaaishaji katika lugha ya kiswahili ni kiambishi/ ki/. Kiambishi / ki/ kinapowekwa pamoja na vivumishi ambavyo mizizi yao inaanzia na irabu ‘u’ ukaakaishaji hutokea
mfano
vivumishi vimilikishi
-angu- ki+angu- kyangu- chyangu- changu
-etu- ki+etu- kyetu- chyetu- chetu
Katika kanuni hii kizuiwa hafifu/k/ ambacho hutamkiwa kwenye kaakaa laini hubadilika kuwa kuzuiwa kwamizwa / ts/ ambacho hutamkwa kwenye kaakaa gumu.
Ukaakaishaji katika nomino, hutokea katika nomino chache za Kiswahili
Mfano
-ki+akula- kyakula- chyakula- chakula
-ki+ombi- kyombo- chyombo- chombo
Ukakaishaji katika vitenzi, hutokea pale ambapo mofu {ki} inapowekwa pamoja na mofu {o} ya urejeshi.
Mfano
{A} + {li} + {ki} + {o} + {ki} +{let} +{a}
1                  2         3       4         5         6           7
{A}+{li} + {cho}_ {ki}+ {let} + {a}   ambapo {ki} + o  cha
1       2                   3      4        5      6
Mofu ya tatu {ki} na ya nne {o} zinaungana na wakati  huohuo panatokea ukaakaishaji ambapo /k/ ina kaakaishwa na kuwa /ts/
Usilimisho pamwe wa nazali kanuni hii inahusu maathiriano ya mofimu zinazofuatana. Maathiriano haya huzifanya mofimu zifanane zaidi kuliko zikiwapelekee katika lugha ya Kiswahili ngeli ya 9, 10 na 11. Ngeli ya 9 umoja naya 10 uwingi  hujulikana kama ngeli ya nazali au kingo’n go. Ngeli ya 11 umoja uwingi wake ni ngeli ya 10

Mfano, N+ goma- {ngoma}
             N+ dizi- {ndizi}
             N+ buzi – {mbuzi}
           N+ geli- {ngeli}
           N + bingu – {mbingu}
Mifano hii inaonesha kuwa mofimu ng’ongo ambayo ni /n/ na /m/ hutokea kutegemea na sauti inayoanza katika mzizi Rubanza (1999) .
Vilevile Mgullu(1999) anajadili usilimisho pamwe wa nazali kutegemea usilimisho ambao fonimu jumuishi huupata. Usilimisho huu, hueleza kuwa hutegemea mahali ambapo konsanti inayofuata fonimu jumuishi hutamkiwa. mfano hutokea kama /n/ - /d/ katika maneno, ndizi, ndama, yaani fonimu jumuishi /n/ hutokea kama  /n/ katika maziongira kabla ya /d/
Pia hutokea kama /m/ - /b/ katika maneno mbuzi mbali yaani fonimu jumuishi /n/ hutokea kama /m/ katika mazingira kabla ya /b/. Lakini mtazamo huu una utata haungwi mkono moja kwa moja kuwa /n/, /m/ ni sauti tofauti za mofimu jumuishi moja.  Huenda ikaja kutokea, baada ya uchunguzi, kuwa labda hizi ni fonimu tofauti ambazo labda zina fanana kidogo kwa sababu zote zina unazali.
 Kwa ujumla, michakato inayotumika katika lugha ya kiswahili imesaidia sana katika uundaji wa maneno ili kufanikisha baadhi ya maneno kutamkwa baada ya kutoka umbo la ndani na kwenda umbo la nje ambalo hutokana na lugha mbalimbali za kibantu kutopkana na athari zitokanazo na utamkaji ndizo zimesababisha kutokea kwa kanuni mbalimbali ili kuweza kusababisha matashi na maumbo ya herufi mbalimbali hutamkiwa sehemu yake inayohusika.

 MAREJEO
 Tuki, (2004), kamusi ya Kiswahili sanifu. Oxford University press: Nairobi.
Mgulu, R..S (1999), Mtaala wa Isimu: Fonetiki, Fonolojia na Mofolojia ya Kiswahili. Longhorn Publishers Ltd: Nairobi.
Massamba, D.P.B (2001), Maendeleo Katika Nadharia ya Fonolojia. Taasi ya taaluma za Kiswahili (Tuki): Dar es salaam.
Habwe, J na peter, K (2004), Misingi ya Sarufi ya Kiswahili. Phoenix Publishers: Nairobi.
Massamba na wenzake, (2003), Sarufi Mauumbo ya Kiswahili Sanifu (SAMAKISA) Sekondari na vyuo. Taasisi ya uchungazi wa Kiswahili: chuo kikuu cha Dar- es – salaam.
Rubanza. Y. I (1999), Mofolojia ya Kiswahili, Chuo Kikuu Huria cha Tanzania: Dar es Salaam.


Maoni 11 :