Mofolojia ni taaluma
inayoshughulikia vipashio vya lugha na mpangilio wake katika uundaji wa maneno.
Vipashio hivyo vya lugha huitwa mofimu (Rubanza, 1996).
Mofolojia ni tawi la taaluma
ya isimu ambalo huchunguza maumbo ya maneno na hususani: maumbo ya mofimu.
(Mathews, 1974)
Hartman (1972) anasema kuwa
mofolojia ni tawi la sarufi ambalo hushughuliia na uchunguzi na uchambuzi wa
maumbo, fani na aina zao maneno yalivyo sasa pamoja na histori zao.
Mofolojia huchunguza mofimu
na alomofu zake fulani na jinsi ambavyo hukaa pamoja kuunda maneno mbalimbali
katika lugha zinamotumika (Richard na wenzake 1985).
Kwa ujumla, mofolojia ni
tawi la isimu ambalo huchunguza maneno ya lugha fulani na aina zake za maneno
hasa upande wa upangaji wa mofimu mbalimbali zitumikazo kwa ajili ya kuunda
maneno. Pia wana taalamu mbalimbali wamefasili maana ya maneno kwa mitazamo
mabalimbali kama ifuatavyo.
Tuki, (1970) Neno ni
mkusanyiko wa sauti ambazo huweza kutamukika na kuandikwa kwa pamoja na kuleta
maana.
Massamba na wenzake (2003)
wanafasi neno kwa kutafasili maelezo ya Lynos (1968:194- 208) kuwa neno linawez
kufafanuliwa katika misingi ya kiumbo sauti yaani kwa kuchunguza sauti
zinazounda umbo zima, kiontografia kwa kuchunguza herufi zinazotumika katika
kuliandaka umbo lake, kisarufi kwa kuchunguza kile kinachowakilishwa na umbo
husika katika lugha.
Katika lugha ya Kiswahili,
maumbo ya kimatamshi na ya kimaandishi huweza kuwakilisha umbo moja au maumbo
kadhaa ya kisarufi. Mfano, katika lugha
ya Kiswahili kuna umbo la Kimaandishi kaa. Kisarufi umbo hili linawakilisha
maumbo matatu yenye maana tofauti kama ifuatavyo.
Kaa- tendo la kuketi kitako
Kaa- aina ya samaki
Kaa- kipande cha ukuni chenye moto au kilichochomwa.
Kwa ujumla, neno ni sehemu
ya lugha yenye kituo kidogo mbele na nyuma yake, au kwa maandishi ni jumla ya
herufi zenye maana zilizotengwa kwa nafsi nyuma na mbele.
Maneno katika lugha ya
Kiswahili huweza kuundwa kupitia michakato mbalimbali kama vile kimofolojia, na
kifonolojia, kwa kutumia mchakato wa kimofolojia, neno huweza kuundwa kupita
kanuni mbalimbali kama vile, udondoshaji, uyeyushaji, Muungano wa sauti, nazali
kuathiri konsonanti, konsonanti kuathiri nazali, Ukaakaishaji, usilimishaji au
usilimisho na mchato wa msinyao.
Katika mchakato wa
udondoshaji, kiambishi awali m- ambacho huonekana katika umbo la nje la maneno
kama mu- tu, mu- gonjwa, mu – kanda. Katika kanuni au mchakato huu wa undoshaji.
Irabu “u” hudondoshwa pale inapofuatiwa na konsonanti halisi katika mpaka wa mofimu.
Mfano.
Mu+ tu= mtu
Mu+ gonjwa= mgonjwa
Mu+ kanda= mkanda
Mu + guu = mguu
Mu + china= mchina
Mu+ kulima = mkulima.
Pia irabu ‘u’ inapokalibiana na irabu inayofanana nayo
hubaki kama ilivyo.Mfano
Muumba- muumba
Muumini- muumuni
Muuguzi- muuguzi
Mungwana- muungwana
Muunguja- muunguja.
Mchakato wa uyeyushaji, kanuni hii
hutokea pale irabu inapoandamana na nazali “m” na pale inapokuwa yenyewe. Irabu
‘u’ inapofuatiwa na mofimu inayoanza na irabu inayofanana nayo hubakia jinsi
ilivyo lakini inapofuatiwa na irabu isiyofanana nayo wakati mwingine huweza
kubakia kama ilivyo au huweza kugeuka na kuwa ‘w’ pia irabu ‘I’ huathiriwa na
kanuni hii mfano
Mi+ ake- myaka
Vi+ ake- vyake
Vi+ ao- vyao
Vi+ akula vyakula
Pia katika kanuni hii neon
likitamkwa kwa haraka uyeyushaji huweza kutokea. Mfano;
Mu+e+nde+shaji mwendeshaji
Mu+i+mba+ji mwimbaji
Mu+ema
mwema
Mu+eupe mweupe
Katika kanuni hii iwapo kuna namna
mbili za utamkaji inaashiria kuwa katika mazingira hayo kanuni ya uyeyushaji ni
ya hiyari.
Machakato wa muungano wa sauti,
kanuni hii hutokea pale ambapo irabu ya mofimu moja inapokabiliana na irabu ya
mofimu nyingine irabu hizo mbili huungana na kuzoa irabuy moja tu mfano
Wa+ ingi- wengi
Me +ingi- mengi
Hapa ina maana kuwa irabu ‘a’ na
irabu za mbele yaani ‘i’ na ‘e’ zinapokutana katika mpaka wa mofimu huungana na
kuzaa irabu moja tu ‘e; lakini kuna vigaili amabapo hutokea inapokuwa mofimu inayoiandama
ina minyambuliko. mfano
Wa+ igi+za+ ji - waigizaji
Wa+ oko+ a+ ji-
waokoaji
Mchakato wa nazali kuathiri konsonanti
andamizi, katika kanuni hii baadhi ya sauti ambazo huathiriwa na nazari
inapokuwa sauti hizo zinazoindamia nazari hizo. mfano.
n+
limi- {ndimi}
n+ refu- {ndefu}
Katika mifano hii inaonekana kwamba
sauti/ l/na/r/ zinapotanguliwa na nazari “n” hugeuka na kuwa sauti/d/
Mchakato wa konsonanti kuathiri nazali,katika
lugha za kibantu umbo la nazali huathiriwa na konsonanti inayoind amia. kwa
mfano
Nguzo- [inguzo]
Ngao-[ ingao ]
Katika mifano hii konsonanti
inayofuatia nazali ni “g”. konsonsanti hii hutamkiwa nyuma kwenye kaakaa laini, kwa maelezo haya…..
haitokei hivihivi bali ni kutokana na kanuni hii maalumu ya lugha nyingi za
kibantu ambazo ni kanuni ya konsonanti kuathiri nazali.
Mchakato wa ukaakaishaji wa fonimu, hutopkea wakati ambapo fonimu zisizo za kaakaa
gumu zionapobadilika na kuwa fonimu za kaakaa gumu. Katika lugha ya kiswahili
fonimu za kaakaa gumu ni mbili yaani vizuiwa kwamizwa ambavyo ni ?t? na ?ts?
kwa hiyo katika lugha ya kiswahili ukaaishaji wa fonimu hutokea wakati ambapo
fonimu zisizo vizuiwa kwamizwa hubadilika na kuwa vizuiwa kwamizwa. Ukaakaishaji
katika lugha ya Kiswahili hutokea zaidi katika vivumishi, nomino na vitenzi .
ukaakaishaji katika vivumishi hutokea katika mipaka ya mofu za vivumishi, vivumishi vinavyohusika ni vile
ambavyo mizizi huanzia na irabu. Kiambishi awali pekee ambacho husababisha
ukaaishaji katika lugha ya kiswahili ni kiambishi/ ki/. Kiambishi / ki/
kinapowekwa pamoja na vivumishi ambavyo mizizi yao inaanzia na irabu ‘u’ ukaakaishaji
hutokea
mfano
vivumishi vimilikishi
-angu- ki+angu- kyangu- chyangu- changu
-etu- ki+etu- kyetu- chyetu- chetu
Katika kanuni hii kizuiwa hafifu/k/
ambacho hutamkiwa kwenye kaakaa laini hubadilika kuwa kuzuiwa kwamizwa / ts/
ambacho hutamkwa kwenye kaakaa gumu.
Ukaakaishaji katika nomino, hutokea
katika nomino chache za Kiswahili
Mfano
-ki+akula- kyakula- chyakula-
chakula
-ki+ombi- kyombo- chyombo- chombo
Ukakaishaji katika vitenzi, hutokea
pale ambapo mofu {ki} inapowekwa pamoja na mofu {o} ya urejeshi.
Mfano
{A} + {li} + {ki} + {o} + {ki} +{let} +{a}
1
2
3 4 5 6 7
{A}+{li} + {cho}_ {ki}+ {let}
+ {a} ambapo {ki} + o cha
1
2 3 4
5 6
Mofu ya tatu {ki} na ya nne {o} zinaungana na wakati huohuo panatokea ukaakaishaji ambapo /k/ ina
kaakaishwa na kuwa /ts/
Usilimisho pamwe wa nazali kanuni hii
inahusu maathiriano ya mofimu zinazofuatana. Maathiriano haya huzifanya mofimu
zifanane zaidi kuliko zikiwapelekee katika lugha ya Kiswahili ngeli ya 9, 10 na
11. Ngeli ya 9 umoja naya 10 uwingi hujulikana kama ngeli ya nazali au kingo’n go.
Ngeli ya 11 umoja uwingi wake ni ngeli ya 10
Mfano, N+ goma- {ngoma}
N+ dizi- {ndizi}
N+ buzi – {mbuzi}
N+ geli- {ngeli}
N + bingu – {mbingu}
Mifano hii inaonesha
kuwa mofimu ng’ongo ambayo ni /n/ na /m/ hutokea kutegemea na sauti inayoanza
katika mzizi Rubanza (1999) .
Vilevile Mgullu(1999)
anajadili usilimisho pamwe wa nazali kutegemea usilimisho ambao fonimu jumuishi
huupata. Usilimisho huu, hueleza kuwa hutegemea mahali ambapo konsanti inayofuata
fonimu jumuishi hutamkiwa. mfano hutokea kama /n/ - /d/ katika maneno, ndizi,
ndama, yaani fonimu jumuishi /n/ hutokea kama
/n/ katika maziongira kabla ya /d/
Pia hutokea kama
/m/ - /b/ katika maneno mbuzi mbali yaani fonimu jumuishi /n/ hutokea kama /m/
katika mazingira kabla ya /b/. Lakini mtazamo huu una utata haungwi mkono moja kwa
moja kuwa /n/, /m/ ni sauti tofauti za mofimu jumuishi moja. Huenda ikaja kutokea, baada ya uchunguzi, kuwa
labda hizi ni fonimu tofauti ambazo labda zina fanana kidogo kwa sababu zote
zina unazali.
Kwa ujumla, michakato inayotumika katika lugha
ya kiswahili imesaidia sana katika uundaji wa maneno ili kufanikisha baadhi ya
maneno kutamkwa baada ya kutoka umbo la ndani na kwenda umbo la nje ambalo
hutokana na lugha mbalimbali za kibantu kutopkana na athari zitokanazo na
utamkaji ndizo zimesababisha kutokea kwa kanuni mbalimbali ili kuweza
kusababisha matashi na maumbo ya herufi mbalimbali hutamkiwa sehemu yake
inayohusika.
MAREJEO
Tuki, (2004), kamusi ya Kiswahili sanifu. Oxford University press:
Nairobi.
Mgulu, R..S (1999), Mtaala wa Isimu: Fonetiki, Fonolojia na Mofolojia ya
Kiswahili. Longhorn Publishers Ltd: Nairobi.
Massamba, D.P.B (2001), Maendeleo Katika Nadharia ya Fonolojia. Taasi ya
taaluma za Kiswahili (Tuki): Dar es salaam.
Habwe, J na peter, K (2004), Misingi ya Sarufi ya Kiswahili. Phoenix
Publishers: Nairobi.
Massamba na wenzake, (2003), Sarufi Mauumbo ya Kiswahili Sanifu
(SAMAKISA) Sekondari na vyuo. Taasisi ya uchungazi wa Kiswahili: chuo kikuu cha Dar- es – salaam.
Rubanza. Y. I
(1999), Mofolojia ya Kiswahili, Chuo
Kikuu Huria cha Tanzania: Dar es Salaam.
rejea nyingine kama ya mathew 1974, richard na wenzake 1985 ujazionesha katika marejeleo
JibuFutaMeshack jackson
FutaIPO vizuri
JibuFutaKazi nzuri sana
JibuFutaKazi nzuri sana
JibuFutaIko vizuri mwalimu
JibuFutaKazi safi
JibuFutaAsante kwa toleo hill nimepata kuelewa vizuri mifanyiko ya kimofolojia katika mabadiliko ya lugha
JibuFutaIna msaada sana ktk ujifunzaji
JibuFutaKazi zuri sana
JibuFutaNaomba kujua michakato kama hivi 6 ya kimofolojia
JibuFuta